Quantcast
Channel: CHUMA BLOG
Viewing all 2614 articles
Browse latest View live

Serikali Yaridhia Utekelezaji Wa Ujenzi Wa Mradi Wa Bomba La Mafuta

$
0
0
CHUMA BLOG

SERIKALI ya Tanzania imeridhia rasmi utekelezaji wa mradi ujenzi wa bomba la mafuta ghafi kutoka Kabaale katika Wilaya ya Hoima nchini Uganda hadi bandari ya Tanga nchini Tanzania. 
 
Uamuzi huo umefikiwa katika Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika  tarehe 29 Septemba, 2016  Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli. 
 
Taarifa ya kuridhiwa rasmi kwa mradi huo imetolewa naWaziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa ambaye amesema ujenzi wa mradi huo utakaoanza wakati wowote kuanzia sasa unatarajiwa kukamilika mwaka 2020. 
 
Amesema ujenzi wa bomba hilo unatarajiwa kugharimu dola za Marekani Bilioni 3.5 ambapo kati yake Dola Bilioni 3 zitatumika kujenga bomba upande wa Tanzania. 
 
Mradi huo mkubwa utatekelezwa kwa ubia wa ujenzi na uendeshaji kwa kushirikishaka mpuni za Total ya Ufaransa, CNOOC ya China, Tullow ya Uingereza na Serikaliza Tanzania na Uganda. 
 
Mhe. Majaliwa ameongeza kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilometa 1,443 linatarajiwa kusafirisha mapipa 200,000 kwa siku ambapo kila pipa litaliingizia taifa Dola za Marekani 12.2. 
 
Amebainisha kuwa pamoja na kusafirisha mafuta ya kutoka nchini Uganda bomba hilo pia linatarajiwa kusafirisha mafutakutoka nchi nyingine zaJ amhuri ya Kidemokrasia ya Congo na Sudani Kusini ambazo zimeonesha nia ya  kusafirisha mafuta yao kupitia bandari ya Tanga. 
 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametaja faida nyingine ambazo Tanzania itazipata kutoka na namradi huo kuwa ni kupatika na kwa ajira zaidi ya 15,000 wakati wa ujenzi na ajira 2,000 baadaya ujenzi kukamilika, kuimarika kwa mahusiano ya kidiplomasia, kukuza biashara katika ukanda wa kaskazini mwa Tanzania, kampuni za ujenziza Tanzania kupata kazi za ujenzi. 
 
Aidha, amesema Tanzania inatarajia kunufaika zaidi kwa kutumia bomba hilo kupitisha mafuta yanayotarajiwa kupatikana katika maeneo ya ziwa Tanganyika na Ziwa Eyasi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMATANO, SEPTEMBA  28, 2016 

Kwaheri Shimon Peres Na Safari Ndefu Ya Kisiasa Israel

$
0
0
CHUMA BLOG 
peres12Marehemu Shimon Peres enzi za uhai wake.
Septemba 13, 2016 vyombo vingi vya habari duniani kote vilitawaliwa na habari ya kuugua ghafla kwa mwanasiasa nguli wa nchini Israel, Shimon Peres.
Mzee huyu wakati akikimbizwa Hospitali ya Sheba Medical Center, alikuwa na miaka 93 na alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya kiharusi yaliyopelekea kuvuja kwa damu kwenye ubongo.
peres…Akiwa kwenye moja ya makongamano ya kimataifa. 
Jopo la madaktari lililoongozwa na daktari bingwa, Dkt. Itzik Kreiss walijitahidi kuokoa maisha ya kiongozi huyu pasipo mafanikio, hatimaye usiku wa tarehe 27 Septemba, 2016 alifariki dunia baada ya mwili wake wote kupooza.
Historia yake
Shimon Peres, alizaliwa Agosti 2, 1923 huko Wiszniew, Poland. Kwenye familia yao walikuwa wawili, yeye na mdogo wake Gershon.
Baba yake Yitzhak alikuwa mfanyabishara na mama yake Sara alikuwa mfanyakazi wa maktaba.
Anahesabika kama mmoja wa wanasiasa wa muda wote kwenye taifa la Israel, wengi wanamuona kama baba wa pili wa taifa hilo baada ya David Ben Gurion, aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa taifa hilo na ambaye anahesabika kama baba wao wa taifa.
Wakati wa uhai wake amewahi kutumikia nafasi mbalimbali nyeti serikalini.
Aliingia kwenye siasa rasmi mwaka 1959 baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Knesset, mwaka 1974 aliteuliwa na Waziri Mkuu wa wakati huo Yitzhak Shamir kuwa waziri wa usafirishaji nafasi aliyodumu nayo kwa muda wa miaka mingi.
Mwaka 1984 aliteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi chini ya Waziri Mkuu, Yitzhak Shamir.
Aliporejea madarakani Yitzhak Rabin, mwaka 1992 aliteuliwa kuwa waziri wa mambo ya nchi za nje hadi mwaka 1995 alipochaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa Israel.
peresi…Akisisitiza jambo enzi za uhai wake.
Akiwa Waziri wa Mambo ya Nje alifanikisha mazungumzo ya amani kati ya Israel na mamlaka ya Palestina hali iliyopelekea kutangazwa kama mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel mwaka 1994.
Amewahi kuwa Waziri Mkuu kwa vipindi viwili tofauti na baada ya kuachia nafasi hiyo alichaguliwa kuwa Rais wa taifa hilo kutoka mwaka 2007 – 2014.
Ametumia miaka 55 akifanya kazi mbalimbali serikalini. Alikuwa mmoja wa viongozi wa juu wachache kuwahi kutumikia nafasi zote muhimu kwenye taifa hilo.
Ameacha watoto watatu Zvia, Yoni na Chemi, mkewe Sonya Gelman alifariki dunia mwaka 2011.
shimon…Akiwa kwenye moja ya dhifa za kitaifa kipindi akiwa Rais wa Israel.
Baadhi ya tuzo alizoshinda enzi za uhai wake.
1994- Tuzo ya amani ya Nobel.
2008- Alitunukiwa Udaktari wa sheria kutoka Chuo Kikuu cha King’s College London.
2012- Tuzo ya Presidential Medal Of Freedom kutoka kwa Rais Barrack Obama wa Marekani.
Marehemu Shimon Peres atazikwa kesho Ijumaa na atapewa heshima zote.
Viongozi mbalimbali duniani wanatarajia kuhudhuria mazishi hayo, miongoni mwao ni Rais wa Marekani Barrack Obama; Katibu Mkuu UN Ban Ki-moon; Kansela wa Ujerumani Angela Merkel; Rais wa Ufaransa Francois Hollande; Waziri Mkuu wa Canada Justin Trudeau; Waziri Mkuu wa Australia Malcolm Turnbull na Rais Wa Mexico Enrique Pena Nieto.

Waziri Mkuu apokea misaada zaidi ya kuwasaidia waathirika wa tetemeko Kagera

$
0
0
CHUMA BLOG

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea zaidi ya sh. milioni 760 zikiwa ni misaada kwa wananchi walioathirika na tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Septemba 10, mwaka huu.
 
Amepokea misaada hiyo kutoka kwa taasisi na wadau mbalimbali likiwemo kundi la wanawake New Millennium linaloundwa na wake wa viongozi wa Serikali walio madarakani na waliostaafu.
 
Makabidhiano ya michango hiyo, yamefanyika jana jioni (Alhamis, Septemba 29, 2016) kwa nyakati tofauti kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam pamoja na makazi ya Waziri.
 
Miongoni mwa waliokabidhi misaada hiyo ni pamoja Meya wa jiji la Dar es Salaam Mhe. Isaya Mwita sh. milioni 10, Kampuni ya mabati ya ALFA imekabidhi mabati yenye thamani ya sh. milioni 50 na kampuni ya Bia Tanzania (TBL) sh.milioni 100. 
 
Wengine ni Ofisa Mtendaji Mkuu kampuni ya vinywani baridi ya Pepsi Cola, Bw. Avinash Jha amekabidhi sh.milioni 50, kampuni ya Round Table pamoja na wadau wao sh. milioni 57, kampuni ya Wool Worth  sh.milioni 20 na Jumuiya ya Waislam (FIRDAUS) imetoa viti 15 vya walemavu.

Aidha, kampuni ya Trans Ocean Supplies LTD imetoa sh. milioni 20, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Mhe. Amina Masenza amekabidhi sh. milioni 18.681,Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki Mhe. Shy-Rose Bhanji amekabishi sh. milioni tano.

Pia Chama cha Waagizaji Wakubwa wa Mafuta Tanzania kimekabidhi sh. milioni 415.8, kundi la mtanzao wa kijamii la Whatsapp la Papaso, D’jaro Arungu limekabidhi sh.520,000 na kampuni ya mafuta ya Camel iliyokabidhi mifuko 1,000 ya saruji.

Jumuia ya Wanataaluma ya Vyuo Vikuu vya Umma Tanzania (ASAs) imekabidhi sh. milioni 7.5, Umoja wa Wamiliki wa Maduka ya Dawa Muhimu Tanzania umekabidhi dawa zenye thamani ya sh. milioni tano pamoja na Eric Shigongo wa Global Publisher amekabidhi mabati 500 yenye thamani ya sh. milioni 10.

Waziri Mkuu amewashukuru wadau wote kwa misaada hiyo na kuahidi kuwa Serikali itahakikisha michango hiyo inafikishwa Kagera kwa walengwa.
 
“Tunashukuru sana kwa michango yote. Michango hii ni muhimu na inaonyesha mshikamano wa dhati uliopo. Michango hii inaonyesha kuguswa na mapenzi ya dhati kwa waliopatwa na maafa. Amesema.
 
Akaunti ya maafa imefunguliwa katika Benki ya CRDB yenye Namba. 015 222 561 7300 kwa jina la KAMATI MAAFA KAGERA – Swiftcode: CORUtztz na namba za simu za mkononi zinazotumika kupokea michango hiyo ni 0768-196-669(M-Pesa), au 0682-950-009 (Airtel Money) au 0718-069-616(Tigo Pesa).
 
Tetemeko hilo lililotokea Jumamosi, Septemba 10, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu 17 na wengine 440 walijeruhiwa kati yao watu 253 walifikishwa Hospitali ya Mkoa, 153 walilazwa, 113 walitibiwa na kuruhusiwa na wengine 38 wanaendelea na matibabu ambapo kati yao watu 23 wamefanyiwa upasuaji mkubwa na wanaendelea vizuri.
 
Pia tetemeko hilo limesababisha nyumba 2,063 kuanguka huku nyingine 14,081 zikiwa katika hali hatarishi baada ya kupata nyufa na 9,471 zimepata uharibifu mdogo huku wananchi 126,315 wakihitaji misaada mbalimbali.
 
(mwisho)
IMETOLEWA NA:OFISI YA WAZIRI MKUU

Asilimia 60 wananchi hawataki maandamano

$
0
0
CHUMA BLOG
chadema
TAASISI isiyokuwa na kiserikali ya Twaweza imesema asilimia 60 ya wananchi wanaunga mkono kuzuiwa kwa mikutano ya vyama vya siasa.
Ripoti hiyo iliyotolewa jana Jijini Dar es Salaam ilihusu maoni ya wananchi kuhusu demokrasia, udikteta na maandamano.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa jijini Dar es Salaam jana ilisema matokeo yake yametokana na takwimu zilizokusanywa kutoka kwa wahojiwa 1,602 kati ya Agosti 23 na 29 mwaka huu.
Kwa mujibu wa utafiti huo, asilimia 95 ya wananchi wana uthamini uwezo wa kuikosoa serikali huku wananchi saba kati ya 10 wakisema demokrasia ndio mfumo bora wa utawala.
Utafiti huo pia unaonyesha kuwa asilimia 60 ya wananchi wanakubali kuzuiwa kwa mikutano ya vyama vya siasa ikihusisha asilimia 70 ya wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na asilimia 33 ya wafuasi wa vyama vya upinzani.
Kuhusu ushiriki kwenye maandamano, asilimia 50 wamesema hawako tayari kushiriki huku asilimia 29 wakiwa tayari kushiriki.
Pia asilimia 80 ya wananchi wanasema baada ya uchaguzi vyama vya upinzani vikubali kushindwa na visaidiane na serikali kuijenga nchi.
Mbali na hilo asilimia 49 wanasema mikutano baada ya kipindi cha kampeni hukwamisha maendeleo huku asilimia 47 wakisema vyama vya upinzani viruhusiwe kufanya mikutano yao bila kipingamizi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze akizungumzia utafiti huo alisema, “Watanzania wengi wanauunga mkono mfumo wa demokrasia ya vyama vingi na uhuru wa kukusanyika na kutoa maoni. Kwa sasa, idadi kubwa ya wananchi hawakubaliani na kauli inayosema kuwa Rais Magufuli ni dikteta.”
Akizungumzia utafiti huo, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeuponda utafiti huo kikisema kuwa taasisi hiyo inaidanganya dunia.

Taarifa kuhusu kesi ya viongozi waliofungua akaunti bandia ya maafa Kagera

$
0
0
CHUMA BLOG
Watumishi  watatu wa Serikali akiwamo Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Bukoba, wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Bukoba wakituhumiwa kutaka kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu.

Watumishi hao wanadaiwa kutaka kujipatia fedha hizo baada ya kufungua akaunti feki iitwayo kamati ya maafa Kagera kwa ajili ya kukusanya fedha za kusaidia waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea mkoani Kagera Septemba 10 mwaka huu.

Watumishi waliofikishwa mahakamani hapo jana ni aliyekuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera, Amantus Msole, Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Kelvin Makonda, Mhasibu wa Mkoa wa Kagera, Simbaufoo Swai na Meneja wa CRDB tawi la Bukoba, Carlo Sendwa.

Akisoma mashtaka hayo, Wakili wa Serikali, Hashimu Ngole, alidai watuhumiwa hao wanashtakiwa kwa makosa mawili.

Alilitaja shtaka la kwanza kuwa ni kula njama za kutenda kosa la kufungua akaunti feki yenye jina linalofanana na jina la akaunti iliyofunguliwa na Serikali kwa ajili ya waathirika wa tetemeko la ardhi.

Aliitaja akaunti hiyo kuwa ni yenye jina la Kamati Maafa Kagera yenye namba 015225617300.

Kwa mujibu wa wakili huyo, watuhumiwa hao badala ya kutumia akaunti ya Serikali kukusanya fedha za maafa, walifungua akaunti yao waliyoipa jina la Kamati Maafa Kagera yenye namba 0150225617300.

Alilitaja shtaka la pili kuwa ni watuhumiwa kutumia madaraka na vyeo vyao vibaya kinyume cha sheria.

Mawakili wanaowatetea watuhumiwa hao walimwomba hakimu awapatie dhamana wateja wao kwa kuwa bado ni watumishi wa Serikali na wanao uwezo wa kujidhamini wenyewe na hawawezi kutoka nje ya Kagera.

Washtakiwa hao walirejeshwa rumande ambapo kesi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo Septemba 30 na hakimu atatoa maamuzi kuhusu dhamana yao.

Waziri Mkuu Kuhamia Dodoma Leo

$
0
0
CHUMA BLOG
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa, anatarajia  kuhamia rasmi Dodoma leo.

Majaliwa anahamia mjini hapa ikiwa ni sehemu ya kutekeleza ahadi ya Serikali ya awamu ya tano ya kuhamia Dodoma ambako ndiko yaliko makao makuu ya nchi.

Julai 25 mwaka huu, katika kilele cha siku ya mashujaa kilichofanyika mkoani hapa, Waziri Mkuu Majaliwa alisema ifikapo Septemba mwaka huu, Serikali itakuwa imehamia mjini hapa.

Hatua hiyo ya  waziri mkuu   ilitangazwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alipozungumza  na waandishi wa habari.

Alisema   Waziri Mkuu anatarajiwa kuwasili leo mchana akitokea   Dar es Salaam alikokuwa akiishi.

“Baada ya kuwasili hapa  atafanya ziara ya siku mbili katika Manispaa ya Dodoma Oktoba mosi na Oktoba 2 mwaka huu   kukagua hatua mbalimbali za maandalizi ya kupokea   Serikali mkoani hapa.

“Wakati wa ziara hiyo, atakagua majengo ya Serikali, maeneo ya kutolea huduma za afya, kituo cha umeme cha Zuzu, masoko, chanzo cha maji Mzakwe na maeneo ya viwanda.

“Kwa hiyo  maandalizi yote muhimu kwa ajili ya mapokezi ya waziri mkuu yamekamilika na uongozi wa mkoa unaendelea kuwajulisha wananchi na wadau wote katika maeneo yatakayohusika na ziara hiyo, washiriki kwa ukamilifu.

“Kwa niaba ya uongozi wa Mkoa wa Dodoma, tunampongeza Waziri Mkuu Majaliwa kwa kuitikia na kutekeleza uamuzi wa Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais John Magufuli kwa kuhamia makao makuu mjini hapa,”

Makamu Wa Rais Kuongoza Upandaji Miti

$
0
0
CHUMA BLOG
makonda-2Mkuu wa Mkoa wa Dar es Saalam Paul Makonda.
MAKAMU wa Rais, Samia Hassan Suluhu anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika
uzinduzi wa Kampeni ya Upandaji Miti Mkoa wa Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar leo, mkuu wa mkoa huo, Paul Makonda amesema kila mwananchi wa Dar anapaswa kupanda mti mmoja kwa ajili ya ustawi wa afya na mazingira.
Amesema zoezi hilo litazinduliwa rasmi na Samia Suluhu katika Barabara ya Kilwa kwenye Wilaya ya Temeke na baadaye watakagua miundombinu
ya maji kwa ajili ya umwagiliaji wa miti hiyo.

Makonda amesema miti hiyo itakayopandwa ni faida ya Mkoa wa Dar kwa ajili ya hewa pamoja na vivuli vya kupumzika hivyo amewataka wananchi kupanda miti yao katika maeneo yanayowazunguka pamoja na
watendaji wote wa mitaa na kata wa mkoa wa Dar.

Diamond Ataja Bei ya Kuuza Page yake ya Instagram Yenye Followers Milion 2

$
0
0
CHUMA BLOG
AKIONGEA KUPITIA KITUO CHA TELEVISION CHA CLOUDS TV KUPITIA KIPINDI CHA SHILAWADU ,ALIULIZWA SWALI KUHUSU GHARAMA YA PAGE YAKE KAMA AKITAKA KUIUZA..BILA KUTAFUNA MANENO DIAMOND ALISEMA PAGE YAKE ANAWEZA KUUZA KWA BEI YA DOLA MILIONI 2 SAWA NA TSH BILIONI 4 ZA KITANZANIA.

Picha : Wenzi mbilikimo waliozaa "Mbilikimo" maradufu Uingereza wafunga ndoa.

$
0
0
CHUMA BLOG

SI mbilikimo tu..!!  Bali Laura Whitfield (26) mwenye urefu wa futi  4 na nchi 2 pekee,ni Mwenza wa Nathan Phillips (37) mwenye urefu wa futi 3 na na nchi 11.

 Raia hao wa Uingereza  waliochumbiana kabla kuzaliwa kwa mtoto wao Nathan Jr,ambae uchunguzi wa kitabibu ulieonesha kuwa mtoto wao ana umbilikimo mara dufu ukilinganisha na wazazi wake kutokana na kuwa na aina mbili za umbilikimo, yaani"anachondaplasia" kama Mama yake na "pseudochondaplasia" kama Baba yake.

                                      Nathan Jr.

Kutokana na hali hiyo, Madaktari walitabiri Mtoto huyo kufariki saa chache baada ya kuzaliwa.
Lakini wahenga walisema; ‘Mungu si Athumani,’ kwani Nathan Jr.kwa sasa ana umri wa miaka miwili na nusu na alikuwa mshika pete wa ndoa ya wazazi wake hao,katika sherehe iliyofanyika kwenye hoteli ya South Causey na kuhudhuiwa  na ndugu na marafiki wa karibu 50.

Kwa mujibu wa mtandao wa Telegraph Wenza hawa awali walikutana wakati wakicheza shoo ijulikanayo"Snow White" na walifunga ndoa kanisani  ambapo Bibi harusi Laura aliambatana na  mwanae na Mumewe kuelekea kanisani akiwa amevalia gauni lenye thamani ya pauni 800 sawa na Sh milioni 2.4.

Makala : Oparesheni Entebbe, Steringi Alifia Uwanja Wa Mapambano

$
0
0
CHUMA BLOG
airbus_a300b4-203_air_france_an0792167
 Air France.
Juni 27, 1976 ndege ya Ufaransa ‘Air France Flight 139’ ikiwa na abiria 248 ndani yake ilitekwa na magaidi  wanne. Ambao walikuwa Wapalestina 2 na Wajerumani 2 baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa Athens, Ugiriki.

Magaidi wa Kipalestina walitumwa na gaidi hatari Wadie Haddad, aliyekuwa kiongozi wa kundi hatari la kigaidi la Popular Front for the Liberation of Palestine–External Operations (PFLP-EO) wakisaidiwa na wenzao waliokuwa wanachama wa kundi jingine hatari la German Revolutionary Cells.
Makundi yote mawili yalikuwa yakiendesha harakati za kupambana na Waisrael popote pale walipo chini ya jua.
Lengo kuu la kuiteka ndege hiyo ilikuwa kuilazimisha serikali ya Israel kuwaachia wafungwa wa Kipalestina zaidi ya 40 waliofungwa nchini Israel pamoja na wengine 13 waliokuwa wakitumikia kifungo katika nchi mbalimbali.
Air France ilianza safari yake jijini Tel Aviv, Israel kuelekea jijini Paris, Ufaransa na baada ya kutua Uwanja wa Ndege wa Athens, Ugiriki magaidi hao wakiwa na silaha za moto yakiwepo mabomu na bunduki waliwalazimisha marubani kubadili safari ya kuelekea Paris na waelekee Entebbe, Uganda kupitia Uwanja wa Ndege wa Benghazi, Misri.
Juni 29, 1976, baada ya kuwa angani kwa muda wa siku mbili hatimaye Air France Flight 139 ilitua uwanja wa ndege wa Entebbe, Uganda zaidi ya umbali wa kilomita 4,000 kutoka Israel.
Dikteta Idd Amin aliwaunga mkono magaidi hao na kuwapa jengo la kuwahifadhi abiria wote 248. Alifanya hivyo kwasasababu kubwa moja alikuwa anataka kuungwa mkono na mataifa makubwa ya kiarabu ambayo yalikuwa na ugomvi na Israel. Aliwapa silaha na askari wa kutosha kuhakikisha hakuna abiria anayetoroka.
idi-aminDikteta Idd Amin.
Baada ya siku mbili tangu kuwasili Entebbe abiria wote walitenganishwa kulingana na utaifa wao. Abiria 148 wasio raia wa Israel waliachiwa na wakabaki abiria 94 wenye uraia wa Israel pamoja na marubani na wafanyakazi wengine 12.
Magaidi walitishia kuwaua mateka wote 96 endapo wafungwa wa Kipalestina hawataachiwa.
TEL AVIV, ISRAEL
waziri Mkuu wa Israel  (wakati huo), Yitzhak Rabin alikutana na kufanya kikao cha siri na Mkurugenzi Mkuu wa MOSSAD, Meja Jenerali Yitzhak Hofi. Kikao hicho cha siri kilifanyika kwenye makao makuu ya MOSSAD jijini Tel Aviv.
prime-minister-yitzhak-rabin-800Yitzhak Rabin.
Ngoja nikueleze jambo moja la muhimu hapa, MOSSAD ni Shirika la Ujasusi la Israel, ni moja ya mashirika ya kijasusi yenye mbinu na ujuzi wa hali ya juu duniani. Wao ndiyo wanahusika na masuala yote nyeti ya kiusalama ya Israel. Wapo wanaoamini MOSSAD ina ujuzi wa juu kuliko hata mashirika ya kijasusi ya CIA (Marekani), M16 (Uingereza) na GRU (Urusi).
mossadMeja Jenerali Yitzhak Hofi (kulia).
Baada ya kikao hicho viongozi hao walikubaliana kupeleka kikosi cha makomando 100 kutoka MOSSAD kwenda kuwakomboa raia wao wakiwa hai na endapo itatokea mmoja wao ameuawa na vikosi vya magaidi basi lazima maiti yake irudi Israel, hawakutaka kuacha kitu Uganda, hawakutaka damu yao ibaki uganda, hawakutaka kumpa Idd Amin kiburi na majigambo.
éöç÷ çåôé  öä"ì òéúåï áîçðäMeja Jenerali Yitzhak Hofi.
Kikosi maalum cha makomando kiliandaliwa chini ya komando wa vita Luteni Kanali, Yonatan Netanyahu ‘Yoni’, kikosi hiki kilipewa jina la Sayeret Matkal kwa maana ya kikosi cha ukombozi na jina la Oparesheni waliipa Code ya Operation Thunderbolt, maana yake Oparesheni Radi.
mosad… Sehemu ya kikosi cha makomando wa MOSSAD.
Baada ya wiki moja ya maandalizi hatimaye usiku wa Julai 4, 1976 ndege za kijeshi ya Israel zikiwa na makomando 100 ndani yake zilianza safari yake ya kuelekea Entebbe, Uganda.
Ndege hizo za kijeshi aina ya Lockheed C-130 Hercules zilikuwa zikiongozwa na rubani ambaye pia ni Komando mwenye cheo cha Luteni kanali, Joshua Shani, kutokana na umbali wa kilometa zaidi ya 4000 kutoka Israel ililazimika kutafuta nchi moja wapo ya Afrika Mashariki ili waweze kujaza mafuta.
rabin-six-day-war2Yitzhak Rabin (katikati) akiwa na baadhi ya makomando.
Ilikuwa ni lazima wajaze mafuta kwasasabu moja kubwa wakati huo ndege zao hazikuwa na uwezo wa kujaza mafuta zikiwa angani. Hivyo ili waweze kwenda na kurudi Entebbe ilikuwa ni lazima wajaze mafuta kabla ya kuwasili Entebbe. Swali likawa wapi watajaza mafuta? kila nchi ilikuwa inamuogopa Idd Amin, hakuna nchi iliyotaka kuingia kwenye mgogoro na dikteta huyu aliyekuwa na vitisho vya kila aina.
Baada ya majadiliano ya muda mrefu Waziri wa Kilimo wa Kenya Bruce MacKenzie alienda ikulu kumuomba Rais Jommo Kenyatta akubali ndege hizo za kijeshi zitue na kujaza mafuta Airspace ambapo leo ndiyo Jommo Kenyatta International Airport.
Ombi hilo lilifanikiwa na MOSSAD walifanya maandalizi yote ya mwisho kutoka Airspace (Jommo Kenyatta International Airport) kwa msaada mkubwa wa MacKenzie ambaye baadaye alikuja kuuawa na vikosi vya Amin.
Julai 4,1976 ndege kubwa ya kijeshi ya Israel, Air Force C-130 ililianza safari ya kuelekea Entebbe. Usiku huu uliobatizwa jina la Oparesheni Radi. Ilielekea Uwanja wa ndege wa Entebbe bila kuonekana kwenye rada za kuongozea ndege. Hapa ndipo uelewe MOSSAD ni majasusi wa hali ya juu.
JINSI ILIVYOKUWA
Ndege hizi za kijeshi zilitoka Israel na kupaa umbali wa mita 30 tu kutoka usawa wa bahari lengo likiwa kukwepa kuonekana kwenye rada za kuongozea ndege kwenye nchi za Misri, Sudan na Saudi Arabia waliokuwa marafiki wa karibu wa Idd Amni.
Baada ya safari ndefu ndege moja kubwa ilitua Nairobi na nyingine ilishika uelekeo wa Entebbe.
Boeing 707 iliyotua Uwanja wa Ndege wa Jommo Kenyatta ilikuwa na madawa ya tiba ya binadamu na nyingine iliyokuwa imebeba makomando ilitua Uwanja wa Ndege wa Entebbe.
Makomando hao waliwasili Entebbe Julai 3 saa tano kamili usiku, wakiwa na ndege hiyo ya kijeshi ya kubebea mizigo, mara mlango mkubwa wa ndege hiyo ukafunguliwa na Mercedes nyeusi na Landlover zinazofanana kwa kila kitu na zile alizokuwa akitumia Dikteta Idd Amin kwenye misafara yake zilishuka kutoka kwenye ndege.
mossadiiMercedes Benz iliyotumiwa na MOSSAD.
Magari hayo yalielekea moja kwa moja kwenye jengo lililohifadhi mateka hao 106. Jengo hili lilikuwa ndani ya uwanja huo wa Entebbe.
Jambo moja ambalo MOSSAD huenda walidanganywa au walipotoshwa ni kwamba hawakujua siku chache zilizopita Idd Amin alikuwa amenunua Mercedes Benz nyingine yenye rangi nyeupe, hivyo walisimamishwa na walinzi wa uwanja huo wa ndege.
Bila kupoteza muda Makomando wa MOSSAD waliwamiminia risasi walinzi hawa kwa kutumia bastola maalum ambazo hazitoi sauti.
Walifanikiwa kuingia na kuwakomboa mateka 102 kati ya 104, bahati mbaya mateka wanne waliuawa.
Kwenye Oparesheni Radi pia kiongozi mkuu aliyewaongoza makomando kuingia ndani ya uwanja wa ndege na kuongoza mapambano ya kuwaua magaidi wote wa nne na kufanikisha ukombozi huo, Luteni Kanali Yonathan Netanyau naye aliuawa baada ya kupigwa risasi kifuani na walinzi wa Idd Amin. Aliuawa wakati akiwasaidia mateka wengine kuingia ndani ya ndege, aliyeumuua naye aliuawa na makomando wa MOSSAD.
yoni-023Luteni Kanali Yonathan Netanyau.
Baada ya kuwabeba mateka na maiti hao ndege hiyo iliondoka na kutua jijini Nairobi ambako ndege nyingine ya kijeshi iliyokuwa na madawa ndani yake ilikuwa inawasubiri.
Majeruhi wote walipatiwa tiba na wengine wawili walikimbizwa Hospitali kisha kupaa hadi Tel Aviv na kupokelewa na mamia ya wananchi.
mossad…Mateka baada ya kuwasili Tel Aviv.
Komando Yonathan Netanyau alizikwa kwenye makaburi ya watu na viongozi maarufu yajulikanayo kwa jina la Mount Herzi.
Oparesheni Radi ilibadilishwa jina na kuitwa Mivitsa Jonathan ‘Operation Jonathan’ maana yake Oparesheni Jonathan.
Naam zilikuwa dakika 90 za mapigano makali Uwanja wa Ndege Entebbe, mahali ambako steringi anaongoza mapamabano na kushinda na yeye kuuawa dakika chache kabla ya kuondoka uwanja wa mapambano.
Hivi ndivyo steringi alifia vitani na Dikteta Idd Amin alifichama kabatini baada ya kupigiwa simu kwamba makomando wa Israel wamevamia na kukomboa mateka wote, mbaya zaidi alidanganywa kuwa sasa makomando hao wanaelekea Ikulu, mahali aliko.

Wema Sepetu Amkataa Idriss Sultan Mchana Kweupeee Pee

$
0
0
CHUMA BLOG
Wema amkataa Idriss Mchana kweupeee pee!!!!!
Ashasema hataki kuwa nae sasa nyie endeleeni kupost ohh shem shem sijui kamuoa dada yenu au???? Watabaki kuwa marafiki kama zamani tuuuu...wema so wamchezo mchezooo...
unalakusema hapo mdau ???Habari ndo hiyooo... Tukutane katika uwanja wa comments. ..

Soma Alichoandika Mtandaoni:


Simba : Mavugo Adai Hukumu ya Yanga Imefika Leo

$
0
0
CHUMA BLOG
SIMBA DAY (2)  Kikosi cha timu ya Simba.
AKIWAKOSA MAVUGO
Kocha Msaidizi wa Simba, Jackson Mayanja, amesema safu yao ya ushambuliaji ipo vizuri na akishindwa kufunga Laudit Mavugo basi Ibrahim Ajibu atafunga leo.

“Takwimu zinaonyesha jinsi safu yetu ya ushambuliaji ilivyo imara kwa kufanikiwa kufunga mabao mengi, tumejiandaa vizuri kupata mabao kwa Yanga na wakijidanganya kumzuia Mavugo asifunge, Ajibu na wangine wapo na wanaiweza kazi hiyo,” alisema Mayanja, raia wa Uganda.

 Straika wa Simba, Mavugo akizungumzia mchezo wa leo, alisema: “Jumamosi (leo) ndiyo itakuwa hukumu ya Yanga kwa sababu nimejipanga kuwanyoosha na kuisaidia timu yangu kupata ushindi.”

1. Vincent Angban
2.Janvier Bukungu
3.Mohammed Hussein ‘Tshabalala’
4.Juuko Murshid
5.Method Mwanjale
6.Jonas Mkude
7.Shiza Kichuya
8.Muzamiru Yassin
9.Laudit Mavugo
10. Ibrahim Ajib
11. Jamal Mnyate

AKIBA: 
 1.Manyika Peter 
2.Hamad Juma 
3.Mohammed Ibrahim 
4. Mwinyi Kazimoto 
5.Novart Lufunga 
6.Said Ndemla 
7.Frederick Blagnon Imeandaliwa na Nicodemus Jonas, Sweetbert Lukonge, Said Ally na Omary Mdose.

Yanga : Pigo Moja Simba Chali Taifa, Cannavaro Nikipangwa Wameisha

$
0
0
CHUMA BLOG
Kikosi cha timu ya Yanga.
Pluijm alisema anataka ushindi ili kupunguza tofauti ya pointi kati yao na Simba kwani wapinzani wao wapo kileleni na pointi 16 wakati wao wapo nafasi ya tatu na pointi 10. “Tunataka kushinda ili kupunguza tofauti ya pointi ndiyo maana mchezo huu ni muhimu kwetu, naamini tutashinda,” alisema Pluijm.
BUSUNGU, MWASHIUYA WAZINGUA
Leo Yanga itamkosa mshambuliaji wake Malimi Busungu na kiungo mshambuliaji Geoffrey Mwashiuya ambao ni majeruhi. Mwashiuya anaumwa goti.


“Mwashiuya na Busungu ndio hawapo fiti asilimia zote kufikia leo (jana Ijumaa), wameshaanza mazoezi lakini ukweli hawapo fiti kwa ajili ya mchezo wa kesho (leo),” alisema Pluijm.
CANNAVARO AKIPANGWA KAZI MNAYO
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ akizungumzia mchezo huo, alisema: “Kama nikipangwa nakuhakikishia Simba watakiona cha moto, waombe nisipangwe tu.”

1.Ali Mustapha ‘Barthez’
2. Juma Abdul
3.Hajji Mwinyi
4.Andrew Vicent
5.Vincent Bossou
6.Mbuyu Twite
7.Simon Msuva
8.Thaban Kamusoko
9.Donald Ngoma
10.Amissi Tambwe
11.Deus Kaseke YANGA SC:
AKIBA: 1.Deogratius Munishi ‘Dida’ 2.Hassani Kessy 3.Oscar Joshua 4.Kelvin Yondani 5.Nadir Haroub ‘Cannavaro’ 6.Haruna Niyonzima 7.Juma Mahadhi

Rwanda Yanunua Ndege Ya Kisasa Ya Airbus

$
0
0
CHUMA BLOG 
rwanda-air-1
Ndege aina ya Airbus A300-200 iliyonunuliwa na Shirika la ndege la Rwanda, Rwandair.
rwanda-air-3
Ndege hiyo ikimwagiwa maji kama ishara ya kupokelewa.
rwanda-air-2
Viongozi mbalimbali wakiwa nje ya ndege hiyo.
rwanda-air-4
Muonekano wa  ndani wa ndege hiyo.
Safari ya kwanza ya ndege hiyo itakuwa kwenda Dubai
Muonekano wa nje wa ndege hiyo.
Shirika la ndege la Rwanda, Rwandair, limezidisha ushindani katika uchukuzi wa ndege Afrika Mashariki na Kati kwa kununua ndege aina ya Airbus A300-200.
Ndege hiyo itawezesha shirika hilo kufika masoko ya Ulaya na bara Asia.
Mkuu wa shirika la Rwandair John Mirenge amewaambia waandishi wa habari kuwa ndege hiyo yenye nafasi ya abiria 244 ndiyo ya kwanza katika ukanda huu na ina teknolojia ya kisasa na ya hali ya juu.
“Ukiwa angani ndani ya ndege hii unaweza kupiga simu, kupata ujumbe wako wa simu, ujumbe wa barua pepe, ujumbe wa WhatsApp na mawasiliano mengine. Haya hayakuwepo katika ndege nyingine tulizo nazo,” amesema.
Ni ndege iliyotengenezwa nchini Ufaransa na kununuliwa kwa kitita cha dolla milioni 200 za Marekani.
Bw Mirenge, anasema safari za shirika la ndege la Rwandair zilikuwa zinajikita sana Afrika magharibi na kati na kwamba ndege hii sasa inakuja kuongeza uwezo wa kuvamia masoko ya Ulaya, Asia na kusini mwa Afrika.
Safari ya kwanza ya ndege hiyo inatarajiwa kufanyika wikendi ijayo tarehe 8 kuelekea mjini Dubai.
Shirika hilo sasa linalenga kusafirisha abiria laki 750 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2017.

LIVE UPDATES: Simba 1 vs Yanga 1 Kutoka Uwanja Wa Taifa

$
0
0
CHUMA BLOG
Dakika ya 46 mpira umeanza, mabadiliko yanafanywa ambapo Kelvin Yondani anaenda benchi na nafasi yake kuchukuliwa na Dante.
Dakika ya 45 mwamuzi Martin Sanya anapiga filimbi kuashiria mpira ni mapumziko, Yanga 1 na Simba 0.
Dakika ya 44 Simba wanaongeza kujituma lakini shuti la Ibrahim Ajibu linatoka nje na kuwa Goal Kick.
Dakika ya 42 Simba wanapata kona baada ya shambulizi kali lililofanywa na Mavugo na kuokolewa na kipa wa Yanga. Kona inapigwa na Mohammed Hussein ‘Zimbwe’ na inatoka nje.
Dakika ya 44 Yanga wanajitahidi kukaba kwa staha huku wapinzani wao wakiwa na presha kubwa baada ya kufungwa goli na mchezaji wao kutolewa kwa kadi nyekundu.
Dakika ya 42 mchezaji wa Yanga Amiss Tambwe anafanyiwa madhambi na refa anampa kadi ya njano mchezaji wa Simba, Mzamiru.
Dakika ya 41 Yanga wanajibu shambulizi kupitia kwa Mahadhi.
Kichuya anafanya shambulizi lakini umakini unamnyima nafasi ya kuipa timu yake goli la kusawazisha.
Dakika ya 36 Donald Ngoma anapiga shuti kali linalodakwa na kipa Angban.
Dakika ya 35 timu ya Yanga wanafanya shambulizi, shuti la Mbuyu Twite linatoka nje.
Dakika ya 30 mpira unaendelea huku mchezaji wa Simba Jonas Mkude kapewa kadi nyekundu baada ya kumtolea maneno machafu mwamuzi.
Mpira umesimama Uwanja wa Taifa, baadhi ya mashabiki  wa Simba wanakimbia kutoka nje ya uwanja, viti vinaendelea kung’olewa upande waliokaa mashabiki wa Simba.
Dakika ya 26 Amis Tambwe anawainua mashabiki wa Yanga anafunga goli la kwanza.
Dakika ya 24 mchezaji Amis Tambwe anafanya faulo na mpira unapigwa kuelekea lango la timu ya Yanga, mpira unatoka nje.
Kelvin Yondani anaongoza ukuta wa Yanga unaokaba kwa kutumia nguvu na umakini, mchezo umejaa kila aina ya ufundi kutoka pande zote mbili.
Yanga wanacheza kwa umakini wa hali ya juu wakikaba kwa pamoja na wanaposhambulia wachezaji wote wanapanda kusaidia..
Dakika ya 16 Yanga wanajipanga na kuingia kwenye eneo la hatari kwa ushirikiano wa Tambwe, Ngoma, Mahadhi… Off side.
Dakika ya 13 shuti la Mavugo linatoka nje.
13Dakika ya 11 mchezaji wa Simba, Mavugo anafanyiwa rafu na kutolewa nje kutibiwa.
Dakika ya 09 Mavugo anapiga mpira wa faulo na kugonga ukuta wa mabeki wa Yanga.
Yanga wanapata kona ya kwanza kwa makosa ya beki.
Kikosi cha timu ya soka ya Simba wameanza kwa kasi kupitia kwa wachezaji wao Kichuya, Mavugo na ajibu bado timu zote zinaviziana.
Mpira umeanza saa kumi kamili. Timu ya Simba wakiwa wamevaa jezi zao za rangi nyekundu na Yanga wamevaa jezi za rangi ya kijani.
simba-2kikosi cha timu ya Simba.
yanga-fckikosi cha timu ya Yanga.

Abdul Kiba Ampa Ujauzito Denti Na Kukataa

$
0
0
CHUMA BLOG

nasra
 Nasra

DAR ES SAALAM: Nasra Salum (19) ambaye ni mwanafunzi wakidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Isqama Islamic Academy iliyopo Oman, amedai kuwa msanii wa Bongo Fleva, Abdul Salehe Kiba, amempa mimba baada yakutembea naye.
Akizungumza ndani ya studio za Global TV zilizopo Bamaga, Mwenge jijini Dar es Salaam juzi, Nasra alisema alikuwa Oman alikokuwa akiishi na shangazi ndipo alipofahamiana na Abdul kupitia Mtandao wa Kijamii wa Instagram.
“Nilikutana na Abdul Kiba kupitia Mtandao wa Instagram, yeye alinitumia meseji na kuniomba namba yangu ya simu nayotumia kwenye Mtandao wa
WhatsApp, nikampa.
“Tukaanza kuchati huku akinitongoza na kunirubuni kwa maneno matamu ya kimapenzi. Nilianza kuichukia shule na
hata kugombana na shangazi yangu, sikutaka shule tena, mawazo yangu yote yalikuwa kurejea nyumbani kuonana na
mchumba wangu mpya.
“Baada ya kugombana na shangazi aliamua kunikatia tiketi kwenye ndege ya Fly Dubai na kurejea nchini kuonana na Abdul,” alisema binti huyo.
Msichana huyo ambaye wazazi wake wote ni wenyeji wa Singida, baba akiwa na asili ya Kiarabu na mama Mnyiramba, alisema baada ya kurejea nchini, alifikia
nyumbani kwa dada yake aishiye Kariakoo jijini Dar es Salaam ambako siku ya pili yake, Abdul Kiba alifika kumtembelea.
“Tangu nikiwa njiani nilikuwa nawasiliana na Abdul, baada ya kufika siku ya pili yake akaja akiwa na rafiki zake watatu, akaniomba niende nyumbani kwake Tabata, nikakubali.
“Tulipofika nyumbani kwake, muda wote nilikuwa chumbani yeye akawa anakaa sebuleni na marafiki zake wakiongea mpaka saa tisa usiku ndipo akarejea chumbani kulala. Tulilala bila kuoga na tulishiriki tendo la ndoa mara nne bila kutumia kinga (kondomu).
“Siku ya pili nilishinda pia kwake na muda wote nilibaki chumbani tu yeye akiwa na rafiki zake sebuleni. Mchana aliniletea chakula, wali kuku, usiku kama
jana yake alikuja kulala saa tisa na tulishiriki tendo la ndoa mara mbili bila kinga.”
Binti huyo alidai kesho yake alirejea kwa dada yake, akimdanganya kuwa alikuwa
Tabata kwa shangazi yake, uongo ambao ulikubalika. Tangu wakati huo, anasema kila akimpigia simu mpenzi wake huyo, hakuwa akipokea kabla ya kuamua kumblock kabisa.
“Niliamua kwenda kupima hospitali maana nilikuwa najisikia kichefuchefu, kukosa hamu ya kula na uchovu muda mwingi. Nikakutwa nina mimba, namtaka Abdul ajisalimishe, kaniharibia
maisha yangu,” alisema.
Global TV ilimtafuta Abdul na kumpa madai yote ambapo alikiri kwa kusema;
“Naomba nikuulize mwandishi, je? Wewe una miaka mingapi? (akajibiwa),
“Hivi inakuingia akilini umpe binti mimba ndani ya siku mbili igundulike? Ni kweli nilifanya mapenzi na huyo binti nyumbani kwangu siku mbili bila kinga. Lakini namuona kama anatafuta kiki kupitia jina langu siamini kama kweli ana mimba.
“Nili-mblock baada ya kuona anasumbua, kila dakika anapiga simu, si kweli kwamba anasoma, yeye aliniambia anafanya biashara Oman ndiyo maana
nilimtongoza. Achane naye.”

 Global Publishers

Magazeti ya Leo Jumapili ya Octoba 2

Waziri Mkuu aeleza mikakata ya serikali kuipanga Dodoma isiwe kama Dar es Salaam

$
0
0
CHUMA BLOG
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imeunda timu ya wataalamu ambao watatoa ushauri juu ya suala zima la kuhamishia makao makuu Dodoma.
 
Ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumamosi, Oktoba 1, 2016) wakati akizungumza na watumishi wa Serikali wa mkoa wa Dodoma, wazee wa mkoa huo, wafanyabiashara pamoja na viongozi mbalimbali kwenye ukumbi wa mikutano wa Dodoma (Dodoma Convention Centre).
 
“Tumeunda timu ya watu 10 ambao ni wataalamu waliobobea kwenye masuala ya ujenzi wa miji mikuu, hawa wana uzoefu wa kuangalia makao Makuu ya nchi yanafananaje. Watakuja Dodoma, wapitie master plan na kisha watapita kwenye maeneo kadhaa ya mji ili waone hali halisi ikoje ndipo watupe maoni yao,” amesema.
 
“Tunataka tusirudie kosa la Jiji la Dar es Salaam la kulazimika kubomoa makazi ya watu kila inapolazimu kufanya uboreshaji wa miundombinu. Hawa watu watatuambia wapi tunatakiwa tuweke njia nne au sita za magari, wapi tuweke bustani au wapi tujenge nyumba za ghorofa moja, mbili, tatu au zaidi,” ameongeza.
 
Akifafanua kuhusu miundombinu, Waziri Mkuu amesema timu hiyo pia itatakiwa kutoa ushauri juu ya wapi ijengwe njia ya malori tu au mahali gani zinahitajika kujengwa barabara za juu (flyovers) ili kuepusha msongamano katikati ya mji wa Dodoma.
 
Bila kutaja majina ya wajumbe wa timu hiyo, Waziri Mkuu amesema timu hiyo itaongezewa wataalamu kutoka China na Malaysia ambao nchi zao tayari zina uzoefu wa kuhamisha makao makuu ya nchi zao zaidi ya mara moja.
 
Alitumia fursa hiyo kuwaeleza watumishi juu ya uwepo wa Tume ya Kuboresha Maslahi ya Wafanyakazi ambayo imekuwa ikifanya kazi tangu mwaka jana. “Kuna vikao vimekuwa vinafanyika tangu mwaka jana baina ya Serikali na viongozi wa vyama vya wafanyakazi kwa lengo la kujadili uboreshaji wa maslahi ya wafanyakazi, na jambo hili linaendelea vizuri,” amesema.
 
Kuhusu madeni ya watumishi wa umma, Waziri Mkuu amewasihi watumishi wawe na imani na Serikali yao kuhusu madeni hayo na kwamba ikimaliza uhakiki unaofanyika hivi sasa, kila mwenye stahili zake atalipwa.
 
Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu ameutaka uongozi wa Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) ihakikishe inakamilisha upimaji wa viwanja 100,000 kama ilivyojipangia ili watumishi hao pamoja na wananchi waweze kupatiwa viwanja haraka iwezekanavyo.
 
“Nimearifiwa kuwa mna mpango wa kupima viwanja 100,000 kwa ajili ya kuwapatia wananchi na watumishi. Kamilisheni utaratibu huo haraka ili watumishi wapewe viwanja na waweze kujenga nyumba zao za kuishi,” amesema huku akishangiliwa.
 
Natambua kuwa mmekubaliana kuanzisha utaratibu wa kuingiza viwanja kwenye mfumo wa kompyuta ili kuepuka double allocation. Harakisheni zoezi hilo ili kama itawezekana, kabla ya Novemba kazi hiyo iwe tayari na watu wapatiwe viwanja chini ya mfumo huo mpya,” amesisitiza.
 
Kuhusu huduma za kijamii kama elimu, umeme, maji na masoko, Waziri Mkuu amewahakikishia watumishi hao kwamba Serikali imeangalia kila eneo na kuzingatia mapendekezo yaliyotolewa ili kuboresha utoaji wa huduma hizo. Amewataka watumishi hao wabadilike na wawe tayari kuwapokea watumishi wenzao watakaowasili kwa awamu kuanzia mwezi huu.
 
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

AMIRI JESHI MKUU RAIS DKT. MAGUFULI ALIPOFUNGA MAFUNZO YA MEDANI YA KIJESHI

$
0
0
CHUMA BLOG

Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiweka saini katika kitabu cha wageni
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein 

Makamanda wakipiga bastola za miali kuashiria kuanza kwa zoezi hilo la medani
Kazi imeanza....
Ndege vita zikiwa katika fomesheni 

Vifaru vinavyotembea majini na ardhini vikikaribia ngome ya adui
Vifaru vinatoka majini na kuendelea na mashambulizi nchi kavu
Makamanda wakiongoza shambulizi
Hali tete ngome ya adui
 
Hatimaye zoezi la kumtoa adui limekamilika kwa mafanikio na wapiganaji wanaelekea uwanja wa sherehe
Wapiganaji wanarudi kishujaa
Wapiganaji wakiwa uwanja wa sherehe
 
Amiri Jeshi Mkuu akiongea na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohamed Shein
 
Mkuu wa Majeshi Jenerali Davies Mwamunyange akikabidhi bendera kwa mpiganaji kuirudisha makao makuu kuashiria hitimisho la zoezi hilo
 
Kwaherini vijana
Amiri Jeshi Mkuu akisalimiana na Mkuu wa wilaya ya Kibaha Mhe. Assumpter Mshama
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiondoka eneo la tukio kwa ukakamavu

Gari Mpya Alilonunua Mchezaji Mbwana Samatta Huku Ubelgiji

$
0
0
CHUMA BLOG
Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta ametumia kiasi cha milioni 130 kununua gari yake ya kwanza nchini Ubelgiji.

Gari hilo alilonunua mchezaji huyo ni Benz Cla220 Cdi AMG Sport 2016 ambayo gharama yake inadaiwa kuwa ni €46,680.

Samatta amechukua uamuzi huo baada ya kufanikiwa kupata leseni inayomruhusu kuendesha gari nchini humo baada ya kunyimwa miezi kadhaa iliyopita.

Inadaiwa kuwa mchezaji huyo analipwa kiasi cha €35,600 kutokana na mkataba wake wa kuichezea timu ya Genk ambao utamalizika mwaka 2020.

Kwa sasa Samatta ameonekana kuwa miongoni mwa wachezaji wa kutegemewa kwenye timu ya KRC Genk ambayo inashiriki kwenye michuano ya Europa League japo amekuwa nje ya uwanja kwa wiki mbili akiuguza majeraha.
Viewing all 2614 articles
Browse latest View live