Quantcast
Channel: CHUMA BLOG
Viewing all articles
Browse latest Browse all 2614

BEKI WA YANGA AKIRI KUWA ANAMHOFIA MAVUGO, ILA KICHUYA ANAMJUA VIZURI SANA

$
0
0
CHUMA BLOG
Image result for mavugo
Beki anayefanya vema kwenye kikosi cha Yanga na ambaye amekuwa akipata nafasi ya kuzanza kwenye kikosi cha kwanza, Andrew Vincent ‘Dante’, amemtolea uvivu kiungo anayesumbua Shiza Kichuya wa Simba kwa kusema kuwa anamjua nje-ndani, hivyo si mtu wa kumsumbua iwapo atapangwa kwenye mchezo wa Oktoba Mosi, mwaka huu wakati miamba ya soka la Bongo, Simba na Yanga zitakapomenyana.


Dante amegeuka lulu ghafla Jangwani kutokana na kiwango cha juu anachokionyesha kwenye safu ya ulinzi katika mechi tano alizoichezea timu hiyo tangu ajiunge nayo akitokea Mtibwa Sugar.
Akizungumza na Championi Jumatano, kuelekea mchezo wa Oktoba Mosi, Dante alisema hana hofu yoyote na ‘kiberenge’ Kichuya ambaye amekuwa tishio kutokana na kasi, chenga na pasi zake kwenye kikosi cha Simba.

 Beki huyo ambaye ni shabiki wa kutupwa wa beki Mbrazili, Dante Bonfim Costa anayekipiga Nice ya Ufaransa alipo mtukutu, Mario Balotelli alisema Kichuya wa Mtibwa ni yuleyule na mbinu zake za kumdhibiti anazijua fika, ila anamhofia sana Mavugo.

Anaomba iwapo atapangwa siku hiyo, apewe kazi ya kumchunga winga huyo waone kama ataweza kufurukuta.

Katika mechi tano hizo alizochezea Yanga, Dante amefanikiwa kucheza sanjari na mabeki wakongwe Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Vincent Bossou na Kelvin Yondani kwenye michezo tofauti.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 2614

Trending Articles